Dennis Shonko kwenye Gazeti la Taifa Leo

@DennisShonko NILIVYODHALILISHWA KWA KUZUNGUMZA LUGHA YA KISWAHILI

interview

Mwalimu na wanafunzi ofisini.

Nakumbuka namna mvua ilikuwa inatunyeshea mchana kutwa tulipokuwa safarini (usiulize tulikuwa na nani. Hayo ni ya siku nyingine). Safari ya kutoka jijini Nairobi kuelekea eneo la *Kiduni. Usishangae kuwa kunyesha kwa mvua hiyo hakukuitia imani yangu baridi. Baridi iliyokusudia kutugeuza kuku aliyenyonyolewa chini ya pepo zitokazo pande zote duniani. Ninachojaribu kusema ni kwamba, nilikuwa katika safari ya kwenda kuonja kipande kingine cha maisha au bora niseme, kuandika ibara nyingine ya maisha yangu.

Baada ya saa kadhaa za kusumbuana na utingo, tulifika katika Chuo cha Ualimu cha *Nira. Ilikuwa mara yangu ya kwanza kuingia humo, sikwambii kufika Kiduni. Watu wachache walikuwa bado wamepiga foleni wakisubiri ima kusajiliwa rasmi chuoni au kuwashika mikono wana wao katika shughuli hiyo nzima. Nilijua sikuwa na kila kitu kilichokuwa kinahitajika; si vitabu si si idadi tosha ya pesa. Ile kauli ya ‘mtu hujikuna ajipatapo’, nilijua haingenifaa wakati kama huo. Nilikuwa kama mbuzi mbele ya hakimu chui! Hebu nisonge mbele kidogo… Continue reading

@DennisShonko UFANISI WA TAMASHA YA KISWAHILI MWAKA WA 2017—BURUBURU

UFANISI WA TAMASHA YA KISWAHILI MWAKA WA 2017—BURUBURU

UFANISI WA TAMASHA YA KISWAHILI MWAKA WA 2017—BURUBURU

Kwa mwaka wa pili mfululizo, Tamasha ya Kiswahili iliandaliwa katika ukumbi wa Huduma ya Maktaba kwa Taifa nchini Kenya (Jumamosi, Oktoba 14, 2017) eneo la Buruburu. Ingawa sikubahatika  kuhudhuria tamasha yenyewe mwaka wa 2016, nilihabarishwa ilivyokuwa yakuigwa.

   Bw Almasi bin Ndangili—ambaye ndiye aliyeibuka na wazo la kuwapo tamasha kama hiyo, ndiye aliyenipa mwaliko. Sawa na wapenzi wengine wa lugha ya Kiswahili, nilifika mapema ukumbini licha ya kukanyaga chechele hapa na pale safarini nikiwa na mwalimu mwenzangu, Peter. Baada ya kitambo kifupi, Bw Ndangili aliyekuwa mratibu na mshereheshaji wa hafla na mwandishi wa tamthilia ya Kifo cha Mwandisi Mmachinga iliyoigizwa hapo baadaye, aliifungua warsha. Stacy alituongoza katika kuuimba wimbo wa taifa. Baadhi ya majina yakutajika yalitambulishwa kwetu k.v Swaleh Mdoe, Bi Pauline Kea, Daktari Hamisi Babusa na Profesa Kineene wa Mutiso waliokuwa wamefika mle. Continue reading

Kasri ya Mwinyi Faud na Adam Shafi Adam

Kasri ya Mwinyi Faud na Adam Shafi Adam

Kasri ya Mwinyi Faud na Adam Shafi Adam

Kasri ya Mwinyi Fuad ni mojawapo wa riwaya maarufu katika fasihi ya Kiswahili. Hii ni riwaya inayosawiri mvutano baina ya ubwana na umwinyi kwa upande mmoj a na unyonge na utwana kwa upande wa pili.
Continue reading

Text Book Centre Jomo Kenyatta Prize for literature 2015, Winners

1) Adult English Category

BOOK: Dust
AUTHOR: Yvonne Adhiambo Owuor
PUBLISHER: Kwani Trust.

Dust

Dust

2) Adult Kiswahili Category

BOOK: Pendo la Karaha
AUTHOR: John Habwe
PUBLISHER: Moran Publishers (EA) Ltd.

Pendo la Karaha

Pendo la Karaha

Continue reading

NASIKIA SAUTI YA MAMA – Tawasifu ya Prof. Ken Walibora

Baada ya tamthilia yake ya pili [MBAYA WETU] kuingia madukani, Prof. Ken Walibora ‘kaibua kitabu kinachoeleza safari ya maisha yake ilovyouwa na inavyozidi kuwa kila jua linapochomoza.

Uketo wa Lugha

“Nasikia Sauti ya Mama” ina uketo wa lugha ya kiswahili inayodhihirisha ukwasi al’onao profesa Ken na mno, weledi wake wa kuyaeleza mengi kwa njia ya kusisimua hivyo kumnata msomaji.

………

Heko kwa wanalonghorn Publishers kwa kujitoma katika hili la tawasifu: NASIKIA SAUTI YA MAMA (Ken Walibora) na “MBALI NA NYUMBANI (Adam Shafi) ni tuzo bora kwetu sote!

NASIKIA SAUTI YA MAMA - Tawasifu ya Prof. Ken Walibora

NASIKIA SAUTI YA MAMA – Tawasifu ya Prof. Ken Walibora

Continue reading

KOPO LA MWISHO NA HADITHI NYINGINE –OMAR BABU (Mhariri)

KOPO LA MWISHO NA HADITHI NYINGINE –OMAR BABU (Mhariri)

KOPO LA MWISHO NA HADITHI NYINGINE –OMAR BABU (Mhariri)

Kopo la mwisho na hadithi nyingine ni mkusanyiko wa hadithi ambazo zimepigwa msasa tena kwa makini naye Omar Babu [Abu Marjan] ambaye ni mshairi na mwandishi wa riwaya na hadithi fupi.

Ni diwani inayoshughulikia maudhui tofautitofauti; Ukabila, siasa. Elimu, mapenzi n.k  … “Ni hadithi zinazoandama mtindo sahili na zinazoashiria masuala yanayomkabili binadamu.”

Kopo la mwisho na hadithi nyingine

Continue reading