Mashetani Wamerudi – Said A. Mohamed
Uzinduzi wa tamthilia hii: Wasta 10-10, 2016

Mashetani Wamerudi Said A. Mohamed
Profesa-Haft-Leo-Wala-Kesho ni mwenye kipaji cha kusema na kuwavuta watu – hasa vijana. Mhusika huyu anatumia kipaji chake kutetea na kupinga ‘mkwamo’ katika Dunia ya Tatu – ikiwemo Afrika. ‘Mkwamo’ huo, ulianza mwanzoni mwa ukolonikale na kushamiri katika ukolonimamboleo. Kwa ajili ya ‘mkwamo’ huo, Afrika imetupwa na kuachwa nyuma kwa kila kitu, hasa katika kunyonywa jana, leo na kesho.
Mashetani Wamerudi ni tamthilia inayoleta mivutano pande mbili: upande wa mashetani na vibaraka vyao, na upande wa vijana na wazee wanaochachamaa. Mwisho wa mvutano, Profesa Hafi-Leo-Wala-Kesho anakufa kifo cha ajabu na kuleta tanzia pamoja na tamaa ya kuamsha silaha ya ukombozi! Tamthilia hii ina mchovyo unaosimamia maana mbili: maana ya kijujujuu yenye lugha ya kificho, na maana ya pill yenye kuleta lugha ya ukinzani na vijembe ndani ya lugha ya mtindo wa usasa, inayoipa hadhira mitazamo mbalimbali kwa wasomaji. Katika mtindo huu, kung vuta nikuvute, mtindo unaoburudisha na kuhuzunisha, inayorambwa ndani ya ‘asali chungu’ na utamu wa mchezo wa sitiari, ishara, mafumbo, usambamba, kejeli na mgao unaofuata mapigo ya ushairi na uwazi wa nathari.
Said A. Mohamed ni mwandishi wa fasihi mwenye ukwasi mpevu na tajriba kubwa. Kazi zake zinajumuisha diwani za mashairi,diwani za hadithi fupi,riwaya na tamthlia.
Pingback: ‘New’ Set Texts for 2017 - My Literature Lesson
nashukuru Mola kutupa shamba lililo dhahania , nalo ni kichwa cha msanii said a.
Kazi njema Said Mohammed. Mimi ni mwalimu mchanga wa lugha shule ya upili ya Mtakatifu Thoma Akuino sehemu ya Kitale Bishop Muge. Nina umri wa miaka 22. Nijuze mtaalamu nahitaji pia kuwa msanii kama wewe naipenda sana lugha na fasihi kwa ujumla. Nifanye vipi?
Hii riwaya mpya yapatikana vipi?
Ni tamthilia
Nazienzi sana tamthilia na riwaya zako Bw. Said na ni katika himaya nzima ya fasihi Afrika.Mwenyezi Mungu akuzidishie maarifa katika ulingo huu wa uandishi.
I really need a copy of this
Uwapi uchambuzi wa Tamthilia hii ya Mashetani Wamerudi?
Hivi karibuni.