@DennisShonko UFANISI WA TAMASHA YA KISWAHILI MWAKA WA 2017—BURUBURU

UFANISI WA TAMASHA YA KISWAHILI MWAKA WA 2017—BURUBURU

UFANISI WA TAMASHA YA KISWAHILI MWAKA WA 2017—BURUBURU

Kwa mwaka wa pili mfululizo, Tamasha ya Kiswahili iliandaliwa katika ukumbi wa Huduma ya Maktaba kwa Taifa nchini Kenya (Jumamosi, Oktoba 14, 2017) eneo la Buruburu. Ingawa sikubahatika  kuhudhuria tamasha yenyewe mwaka wa 2016, nilihabarishwa ilivyokuwa yakuigwa.

   Bw Almasi bin Ndangili—ambaye ndiye aliyeibuka na wazo la kuwapo tamasha kama hiyo, ndiye aliyenipa mwaliko. Sawa na wapenzi wengine wa lugha ya Kiswahili, nilifika mapema ukumbini licha ya kukanyaga chechele hapa na pale safarini nikiwa na mwalimu mwenzangu, Peter. Baada ya kitambo kifupi, Bw Ndangili aliyekuwa mratibu na mshereheshaji wa hafla na mwandishi wa tamthilia ya Kifo cha Mwandisi Mmachinga iliyoigizwa hapo baadaye, aliifungua warsha. Stacy alituongoza katika kuuimba wimbo wa taifa. Baadhi ya majina yakutajika yalitambulishwa kwetu k.v Swaleh Mdoe, Bi Pauline Kea, Daktari Hamisi Babusa na Profesa Kineene wa Mutiso waliokuwa wamefika mle. Continue reading

Homa ya Nyumbani na Hadithi Nyingine : Profesa Ken Walibora na Said A Mohamed.

Kazi mpya..kutoka jiko la Phoenix Publishers… Hadithi 15, waandishi mbalimbali kutoka kote Afrika Mashariki, mkusanyiko huu wa hadithi fupi umehaririwa na Profesa Ken Walibora na Said A Mohamed. Waandishi ni pamoja na Doreen Baingana (Uganda), Patience Onyut (Uganda), Mohammed Ghassani (Pemba), Prof. Ken Walibora, Prof. Said A Mohamed, Prof Farouk Topan, Magayu Magayu na wengineo. Pata nakalayo!

Nukuu: Phoenix Publishers Ltd.

Homa ya Nyumbani na Hadithi Nyingine : Profesa Ken Walibora na Said A Mohamed.

Homa ya Nyumbani na Hadithi Nyingine : Profesa Ken Walibora na Said A Mohamed.

Continue reading

Nyuso za Mwanamke – Said A. Mohamed, 2010

Nyuso za Mwanamke - Said A. Mohamed, 2010

Nyuso za Mwanamke – Said A. Mohamed, 2010

Nyuso za Mwanamke

Said A. Mohamed, 2010

Sasa Sema (Longhorn Publishers)

Msichana Nana

“Nana, msichana mrembo anajipata katikati ya jamii yenye mielekeo ya kumfinyanga mwanamke na kumyumbisha kama kayamba. Kila anayemwona Nana anamchukulia kuwa ni pambo la mji lenye nyuso nyingi au llisilokuwa na uso hata mmoja…” Continue reading

Tamthilia ya ‘AMEZIDI’ na Said A. Mohamed

Tamthilia ya 'AMEZIDI' na Said A. Mohamed

Tamthilia ya ‘AMEZIDI’ na Said A. Mohamed

Ame na Zidi wanajikuta katika umaskini mkubwa katika bahari iliyohaa mali. Katika hali hii ya uhitaji, wanatambua kuwa hawana jingine la kufanya ila kuomba msaada ili wayatosheleze mahitaji yao. Msaada unapokuja, unaleta unaleta madhara mengi zaidi.

Huu ni mchezo mawazoni unaotazama matatizo ya kijamii na ya kiuchumi katika nchi nyingi za kiafrika za hivi leo.

Mwandishi alizaliwa Unguja (Zanzibar) mwaka wa 1947. Alielimishwa huko huko Unguja na baadaye akajiunga na chuo kikuu cha Dar-es- Salaam, na kisha chuo kikuu cha Leipzig, Ujerumani. Amefundisha katika shule za upili na vyuo mbalimbali. Kabla ya ku7hamia Ujerumani, alikuwa Profesa katika Chuo kikuu cha masomo ya kigeni cha Osaka, Ujapani. Continue reading