Ulikuwa uvumi tu! Ufifi!

Jumanne usiku, kila nilipopenyepenya kwenye mitandao ya kijamii niliwaona wengi wakikutajataja. Walikutajataja kwa kile ambacho nilikataa kabisa kuamini. Wengi hatukuamini na hivyo kutugeuza wakosoaji. Tuliwaonya ‘kasuku’ dhidi ya uvumi kuwa ulikuwa umetangulia mbele ya haki. Ili nisiutese moyo wangu nilizima data hadi keshoye Jumatano, 15/4/2020. Nikawa ninachakura kwenye Twitter, Whatsapp na Facebook. ‘Uvumi’ ulikuwa umetamba kote. Sikutaka ya kukisiwa tena! Nilipoiwasha televisheni, duh! Stesheni ya NTV ilikuwa na maandishi haya kwenye kiwambo: